Saturday 26 October 2013

KANUNI ZA KUEPUKA KUZINI NJE YA NDOA AU MPENZI WAKO

Hakunaga na Brother Kalu
Kanuni za kuepuka kuzini nje ya Ndoa au mpenzi wako
Leo tuende moja kwa moja kuangalia baadhi ya mambo ambayo yaweza kukusaidia kuepuka kuzini nje ya ndoa yako au kutoweza kumsaliti mpenzi wako.
1.      Kujiepusha kuwa karibu na jinsi zingine ukiwa umelewa
Hapa nitoe ufafanuzi wa jambo moja la jinsi ambapo nazungumzia masuala ya maumbile ambapo wengi wetu tunachanganya neno jinsi na Jinsia.
Kuepuka kuwa karibu na jinsi tofauti nawe ni suala gumu sana lakini ni vema unapokuwa unakula maji(kilevi) ni vema ukawa makini kuwa mbali na mtu wa jinsi nyingine ili kuepukam kupata vishawishi na kumsaliti mwenzi wako.
2.     Epuka mazungumzo ya kimahaba
Ni njia rahisi sana inayoshawishi watu wengi kujiingiza kwenye usaliti ama mapenzi mapya ambapo endapo hautakuwa makini na kujiingiza katika mazungumzo ya kimahaba na mtu wa jinsi nyingine unaweza kujikuta unajiingiza katika usaliti wa kimapenzi lakini nji hii licha ya kuwa ni njia moja wapo ya kuepuka usaliti ni njia nzuri ya kuanzisha mapenzi mahusiano mapya ambapo wengi hushawishika na kujikuta kutamani kupata vitu vipya katika mahaba ambavyo mtu aliyenaye kwa muda huo amevigusa katika mazungumzo yao.
3.Kuwa mkweli
Ukweli ni jambo muhimu katika kudumisha mahusiano na kuepuka usaliti kwasababu mwenzi wako anaweza kuhisi kitu kuwa umeanzisha mahusiano na mtu mwingine ambaye mara kadhaa mnafanya nae utani, hivyo ni vema ukawa mkweli kwa mwenzi wako kumweleza kuwa mtu huyo mnafanya masihara nae na wala hakuna jambo lolote linaloendelea kimahusiano tofauti na kutumia lugha kama ‘’Kwani unafikiri mimi nafanya nini nae’’ hilo jibu sahihi katika kuboresha mahusiano yenu.
4.Epuka kupigana busu na jinsi nyingine
Kumpiga busu mtu ambaye si jinsi moja nawe ni kichocheo cha usaliti katika ndoa na hata mapenzi ya kawaida kwasababu Mungu aliumba miili yetu katika misisimuko ya aina mbalimbali ambapo mtu mwingine ukimpiga busu bila kujalisha kuwa ni mwanaume au mwanamke hujikuta anasisimuka vibaya sana na kuhisi kuwa angekuwa sitakwa sita nawe kwa muda huo angesisimuka hivyo si vema kufanya hicyo.
5. Usimweleze mtu hisia zako
Epuka kueleza hisia zako za kimahaba kwa mtu asiye wa jinsi yako kwa mfano mtu kagombana na mpenzi wake ama mke/mume wake si vema ukamwambia hisia zako kwake za kutomtenda bali ni vema kumwambia kuwa siyo vizuri kugombana na mwenzi wake na jaribu kutoa ushauri ambao hauna ushawishi wa kumwondoa kwa mwenzi wake.
Hapa sielezi kuwa haupaswi kuwa mkarimu kwa watu la hasha bali nazungumzia kuwa makini na kuepuka kuwa mmoja wa watu wenye historia za kuvunja mahusiano ya watu bali ukiwa mshauri mwema utaheshimika zaidi.
6. Onyesha wajibu wako
Ni vema katika mahusiano kila upande ukaonesha wajibu wake kwa mwenza wake ambapo waweza kumtia moyo mwenzi wako kuwa yeye amekuwa sumaku kwako kwa kukupa faraja na hasa ni mwanamke/Mwanaume  ambaye ulikuwa ukitamani siku nyimgi kuwa naye na hatimaye Mungu kakupa macho ya rohoni kumpata yeye.
Hapa wapo baadhi ya watu ambao si wakweli ambao wanafanya maigizo kutamka maneno kama haya huku wakitoa zawadi ili kuficha mambo yao huo ni usaliti na hapa nasema kuwa haifai….kama upo hivyo jirekebishe acha usaliti.
Mpenzi msomaji wa safu hii ya Hakunaga baada ya kuoina baadhi ya njia ambazo zinzweza kukusaidia kutojiingiza katika usaliti wa mapenzi na ndoa wiki ijayo tutaona nji kadhaa wanazoweza kuzitumia wanawake kuwa sumaku kwa wanaume wao.
Tchao…
Brother kalu

No comments:

Post a Comment